Nchini Kenya, zaidi ya theluthi moja ya watu hukua katika familia za mzazi mmoja.
BBC Africa Eye imefuatilia safari ya kibinafsi ya mwanahabari Namukabo Werungah, ambaye hajawahi kumjua babake na ameamua kutafuta sehemu hii ya utambulisho wake.
Hajui ikiwa yu hai au amekufa, lakini harusi yake inakaribia, ameamua kuwa ni wakati wa kujua historia yake.
Je, atampata mwanaume ambaye alitakiwa kumwita baba? Na ikiwa atafanya hivyo, atamtaka maishani mwake?
#bbcswahili #bbcafricaeye #kenya